UTANGULIZI:
Mpango wa Taifa wa kudhibiti na kuratibu silaha ndogo nchini Tanzania, ni mpango
wa miaka mitano wa uendelezaji wa miradi inayohusisha sekta zote, wenye malengo
ya kuzuia, kudhibiti na kutokomeza uzagaaji haramu wa silaha ndogo. jitihada
za kwanza za mpango huu, na dunia kwa ujumla zimeanzishwa kwa uanzishwaji na
uendelezwaji wa mipango ya utafiti, kuhusisha jitihada za pamoja za kitaifa na
kimataifa na jamii kwa ujumla, katika kupambana na tatizo hili.jitihada hizi
za uendelezaji na utekelezaji wa mpango huu waTaifa zimethibitisha kuwa zitakuwa
bora na zenye mafanikio. Utekelezaji huu umeanza tarehe I februari, 2002.
KWA NINI TANZANIA:
Ukanda wa nchi za Maziwa Makuu ya Afrika zimekuwa ni nchi zinazosumbuliwa na
uzagaaji wa silaha ndogo, pamoja na nchi za Kati, Kusini na Mashariki. Kwa kipindi
cha miaka 50 iliyopita, kutokana na mapambano ya kudai uhuru na ukombozi wa Mwafrika,
eneo hili limeathirika sana.
Eneo hili limeathirika kutokana na vita baridi vilivyokuwa vinaendeshwa, na eneo
lilionekana kama uwanja wa vita. Kutokana na vita baridi hivyo, na mapambano
ya kudai uhuru, kumepelekea kuwepo kwa wanajeshi wengi wenye ujuzi mdogo ambao
waliachwa kutokana na migogoro hiyo. Kuwepo kwa silaha ndogo nyingi pamoja na
risasi kumeliathiri sana eneo hili.
Vyanzo vya upatikanaji wa silaha ndogo katika eneo hili ni vya zamani na vile
vile vipya. Si kwamba silaha zote zilizo katika mzunguko zimesababishwa na sababu
hizo. Kutokana na Kuwepo kwa mchanganyiko wa vyanzo vya kuzagaa silaha haramu,
katika eneo hili, na katika jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ujumla, mpango
madhubuti wa kutokomeza uzagaaji huu unahitajika sana. Zaidi ya hapo, msisitizo
unahitajika kwa serikali ya Tanzania kufanya jitihada za kipekee katika kupambana
na uhalifu, ugaidi na silaha haramu katika nchi za Kusini, Mashariki na Afrika
ya Kati.
Sababu zinazoipa umuhimu nchi ya Tanzania.
- Tanzania ipo katikati ya barabara inayounganisha nchi za Kusini na Mashariki
na kati ya bahari ya Hindi, na nchi za Afrika ya Kati.
-
Tanzania inapakana na nchi zilizo vitani na ambazo zina ugomvi wa kisiasa za
Kusini na Kati.
- Mipaka ya Tanzania imekuwa ikitumika kwa kupitishia silaha haramu
pia imeathirika na ugaidi pamoja na kuongezeka kwa uhalifu.
-
Tanzania, haifungamani na nchi yoyote kisiasa, ni Mwanachama wa SADC, jumuia
ya Afrika Mashariki, SARPCCO na EARPCCO.VilevileTanzania ni nchi imara na yenye
rekodi nzuri katika suala zima la kuwasaidia wakimbizi wa vita.
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekuwa ikishiriki kwa dhati katika jitihada
zote za kitaifa na kimataifa katika kutunga sheria za kupambana na uzagaaji wa
silaha, na biashara haramu ya silaha. Kwa kujihusisha kwake huko, si to kwamba
imetoa mchango thabiti, bali pia imethibitisha kwamba makubaliano yanalenga kwenye
mahitaji yaliyoazimiwa.
Mpango wa utekelezaji wa Itifaki yaVienna,Azimio la OAU la BAMAKO, Itifaki ya
SADC ihusuyo silaha na risasi, Azimio la Nairobi, Itifaki ya Afrika Mashariki
ya Silaha zinazotoa miongozo ya kitaifa na kimataifa na zote zipo katika utekelezaji.
Makubaliano yote haya yanatoa misingi imara ya kisiasa ambayo kwayo yatasaidia
kukabiliana na uzagaaji wa silaha ndogo na yametoa mwongozo mzuri wa uanzishwaji
wa mpango wa taifa waTanzania.
MAAMUZIYA KITAIFA:
Kwa kuwa maamuzi haya ya kitaifa na kimataifa yametoa msingi imara wa kisiasa,
ni ngazi ya kitaifa sasa yenye jukumu la utekelezaji wa mipango hiyo kwa vitendo.
Kwa kujua haja ya haraka ya utekelezaji wa mpango huo, serikali W Tanzania imeanzisha
vyombo vitakavyosimamia utekelezaji wa makubaliano au mipango hiyo.Vyombo vikuu
vitatu vilianzishwa mwaka 2001 ambavyo ni:
- Kamati ya Kitaifa ya silaha ndogo ambayo ni National Focal Point.
- Kamati ya kitaifa
ya kuratibu na kudhibiti silaha ndogo.
-
Na Provincial Task Force ya kuratibu na kudhibiti
Kwa kuanzisha vyombo hivi, Serikali ya Tanzania ilihakikisha kuwa washika dau
wote wanashirikishwa/wanahusishwa.Vile vile Mamlaka za mikoa na mitaa, wakala
wa Serikali na jamii ya Watanzania kwa ujumla ni sehemu muhimu sana kwa vyombo
vyote hivyo vitatu. Baada ya vyombo hivyo vya Serikali kuanzishwa hatua iliyofuata
ya kuendeleza mpango waTaifa ni kuhakiki hali ya silaha ndogo NchiniTanzania.
Kamati yaTaifa ilianzisha mpango thabiti wa kuhakiki hali hiyo NchiniTanzania.
Malengo ya zoezi hilo yalikuwa ni kuona hali, na kiasi cha uzagaaji wa silaha,
kulinganishwa na mahitaji na upatikanaji, uwezo uliopo, na nyenzo zilizopo za
kulielezea tatizo, mtazamo na uzoefu wa Watanzania kuhusiana na uzagaaji wa silaha
ndogo.Taarifa hizi kwa mfano zilipatikana baada ya watu kuhojiwa, kufanya makongamano,
na tafiti mbalimbali zilizofanywa kushirikiana na vyama mbalimbali vya Kitaifa
na Kimataifa visivyo vya kiserikali. Kwa upande mwingine Serikali ilifanya uhakiki
wake kuona uwezo wake kisheria wa kushindwa kuzuia kupenya kwa silaha haramu
kupitia maeneo muhimu yaliyo nchini. Uhusiano na mawasiliano kati ya sekta zote
za kijamii zilizo za kiserikali na sizizo za kiserikali vilikuwa ni vitu vya
msingi katika zoezi hili.
Matokeo ya zoezi hili la Kitaifa yaliipatia Serikali ya Tanzania taarifa muhimu
ambayo ingeweza kutumika katika kurekebisha mfumo kwa ajili ya utekelezaji wa
mpango huo waTaifa, na ikibidi kufanya marekebisho kabisa ya mfumo mzima, au
kuanzisha mfumo mpya. Usanifu wa utekelezaji wa mpango huu wa Taifa uliopatikana
Novemba 2001 ni kama ifuatavyo:
- Kamati ya Taifa ya Ulinzi na Usalama - chombo kikuu cha maanuzi yote yanayohusu
usalama wa Taifa, na ambacho majukumu yake pia yameongezwa ya kudhibiti silaha
ndogo.LI>
Kamati yaTaifa ya silaha na risasi - kamati inayohusisha washikadau wote wa Serikali
ambao wana wajibu wa kulielezea tatizo la silaha ndogo, na ambao shughuli zao
zinaunganisha taasisi za Kimataifa na kikanda, kwa mfano SADC na EAU.
-
Mawakala wa mikoa na kamati ya Taifa - vyombo vya kimikoa vilivyo chini ya kamati
ya Taifa vinavyotekeleza maamuzi ya kamati ya Taifa.
-
Kamati ya Taifa ya kuratibu na kudhibiti silaha ndogo - inayofanya shughuli zake
sambamba na kamati ya Taifa. Kamati maalum ya mipango, inayoratibu, inayohamasisha
michango na kuhakiki mpango wa Taifa. Wajumbe wa kamati hii ni pamoja na Maofisa
Waandamizi wa Polisi, Meneja Miradi na Wawakilishi wa Kitaifa na Kimataifa wa
vyama visivyo vya Kiserikali.
Mbali ya vyombo hivi, Kamati ya Taifa ya kuongeza uwezo wa kifedha imeanzishwa
ili kuhakikisha kwamba
miradi
iliyoanzishwa
inaimarika
kwa
kutumia
uwezo
uliopo
na
kuongeza fungu la fedha lililopo kwa lengo la kuendeleza, katika kipindi cha
miaka mitano,
miradi
imara na inayojitegemea.
MPANGO WATAIFA WA UTEKELEZAJI:
Taratibu zilizoelezewa hapo juu ni vyombo ambavyo utekelezaji wa miradi - madhumuni
ya mpango waTaifa, zinategemewa kwa ajili ya utekelezaji. Mpango waTaifa wa utekelezaji
unahusisha nyanja mbalimbali na miradi ambayo inatekelezwa kwa. pamoja kati ya
Serikali na mawakala wa jumuia za kijamii.
Ratiba ya miradi hiyo imeandaliwa kuhakikisha kuwa utekelezaji wa miradi hiyo
utafanywa kwa usahihi katika kipindi chote cha miaka mitano.
Uanzishwaji wa miradi, kwa ajili ya mpango wa Taifa, umefanywa kwa kuhusisha
maeneo yote, na uhakiki wa sekta zote nchini Tanzania, mwishoni mwa mwaka 2001.
Kila sehemu au mradi una wakala wake na vyama visivyo vya Kiserikali vya Tanzania
vitakuwa na mwakilishi wake atakayehusika moja kwa moja akisaidiwa na wajumbe
wa kamati ya Taifa, mawakala wa Serikali, na vyombo vya kijamii. Kila mradi utafanywa
kwa hatua, zilizothabiti, ambazo zimeandaliwa ili zilingane na uwezo wa kifedha
uliotengwa.
Zaidi ya miradi 100 midogo midogo imethibitishwa kwa ajili ya utekelezaji katika
hatua mbalimbali. Kila eneo/nyanja linalohusu silaha ndogo nchini linapewa kipaumbele.
Hivyo kuna miradi inayoangalia au inayodhibiti hazina ya silaha, na kuimarisha
udhibiti wa mipaka, na kuna He inayojihusisha na kupunguza hali ya utegemezi,
kwa kutoa elimu kwa jamii na kuanzisha shughuli za kiuchumi. Vile vile, si miradi
yote yenye sifa na muonekano wa kitaifa. Miradi mingi imelenga katika kuimarisha
mahusianao kati ya Tanzania na majirani zake na mingine ipo kwa ajili ya kuboresha
uwezo wa sekratariati wa nchi za Kusini na Mashariki ya Afrika kwa kushirikiana
kwa pamoja katika kukabiliana na tatizo la biashara haramu ya silaha.
Hivyo, mpango huu wa Taifa wa Tanzania unajumuisha mfumo muunganifu unaohakikisha
ubora wa udhibiti wa miradi midogo. Miradi hii midogo imetengwa katika sehemu
ndogo ndogo. Sehemu kuu sita za mpango wa Taifa zinaweza kuelezwa kwa. ufupi
kufuatana na mambo yafuatavyo:
- Uanzishwaji/uboreshwaji/uhamasishwaji wa vyombo vya kitaifa na mawakala wake.
Uhakiki wa sheria za nchi, taratibu za kiutawala na utekelezaji wa miongozo mipya.
Mafunzo na uboreshaji uwezo/ufanisi.
-
Kuendeleza ushirikiano wa kitaifa na kimataifa pamoja na kubadilishana taarifa/habari.
-
Kushirikiana na kufanya kazi pamoja na jamii ili kuimarisha mpango wa Taifa na
kuhamasisha ushirikishwaji wa jamii, katika utekelezaji wa mpango huo,
- Kugundua na kuyafanyia kazi maeneo yote sugu, kama vile mipakani.
Miradi yote midogo, inafadhiliwa na mpango wa muda mrefu, ambao unajishuhulisha
na uanzishwaji wa nguvu za pamoja za kulishuhulikja tatizo la silaha ndogo,
uanzishaji wa nyenzo ambazo zitatoa ufafanuzi wa jinsi ya kulitatua tatizo
husika, na utekelezaji
wa mpango wa kuratibu na kudhibiti silaha, ndani na nje ya nchi. Kwa kuwa
na taratibu hizi, Watanzania wanaweza kuchukua hatua maridhawa za kuzuia,
kuondoa, na kutokomeza kabisa tatizo la silaha ndogo kwa njia iliyo bora.
Moja ya vigezo ambavyo, mpango huu wa Taifa unautumia ni kwa kufanya kazi iliyo
sahihi. Matokeo yake ni upatikanaji wa gharama, zilizopatikana katika hatua mbili.
Bajeti ya kwanza ya mradi imepatikana kufuatana na uwezo uliokuwepo kuweza kufadhili
mradi, bila kutegemea ufadhili wa nje. Katika hatua ya pili, uhakiki wa gharama
umefanywa ili kujua ni shughuli gani zingehitaji kuombewa fedha ya ziada. Hata
hivyo, katika hatua zote, gharama za miradi zimekamilishwa na pesa za Serikali.
Kwa misaada toka nje ya nchi, Serikali yaTanzania iliomba kutoka Serikali ya
Uingereza na Ubalozi wa jumuia ya Ulaya.
Serikali ya Uingereza imetoa ongezo la fedha za kuanzia miradi ambao utekelezaji
wake umeanza tarehe I Februari 2002.
HITIMISHO - MAENDELEO BAADAYA MAKUBALIANO:
Mpango wa Taifa wa utekelezaji unaonyesha taratibu za kuzuia, kuondoa na kutokomeza
uzagaaji wa silaha ndogo ni taratibu ambazo zimepatikana baada ya kuwepo mipango
ya pamoja, iliyoonyesha haja ya kushirikisha jamii, ili hali ya amani, usalama
na maendeleo iweze kupatikana. Wakati mpango huu wa Taifa unalenga katika kuratibu
na kudhibiti silaha ndogo, mafanikio yake si to kwamba yatalenga katika silaha
na usalama, lakini pia katika utawala bora wa serikali, demokrasia, uaminifu
na maendeleo, kwani msingi wake umeanzishwa na kutekelezwa na Watanzania, na
utawanufaisha Watanzania wote kwa ujumla.
Kwa maelezo zaidi wasiliana na:
Kamanda wa Kitengo cha Kuratibu na Kudhibiti silaha ndogo,
Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai, S.L.P 9093,
Dar es Salaam. Tanzania,
Simu 255 22 213 2252 au
Mr. Jakkie Potgieter,
Mkurugenzi Safer Africa,
AMAD Appointed Manager
173 Beckett
Street,Arcadia
Pretoria 0083, South Africa
Tel: 27-12-344-6700
Fax: 27-12-344-6708
www.saferafrica.org
Email: safe rafrica@saferafrica.co.tz
Centre of Peace and Economic Development - CEPEDE
1st Floor ZahraTower (MZ02)
Corner of Zanaki and Indira Ghandi Street
Dar es Salaam
Tel: + 255 2 213 6391
Fax: + 255 2 21 213 6393
Email: cepede@africaonline.co.tz